kotii

kotii

TIA YOTE SEHEMU YA 27

SIMULIZI:TIA YOTE

NA:GAO

SEHEMU YA 27

SIMU:0654387935


ILIPOISHIA......... nilishangaa Grace kunifata na kunikumbata huku akilia kabisa tena alivyonikumbata baadhi ya machozi yalinidodea kifuani hata nilipojaribu kumuliza amepatwa na nini aliendelea kulia tu................ ....
ENDELEAAAA.... Kitendo kilebkilinishangaza vya kutosha na kushindwa kupata tafasiri kamili ya kilio cha Grace.

"Grace unalia nini naomba unambie jamani,kipi kinakuliza."

"Gao acha tu yani sijui wanaume mpewe nini,aah najuta"alisema grace hapo kidogo picha ilinijia,na kujua fika ni mapenzi hayo ndio yanamsumbua japo sijajua kwa kina tatizo lake ila nilihisi tu kutokana na maneno yake.

"Wanaume wananini?,Grace"nikamshushia swali.

"Gao mimi siamini kama Ally kanifanyia vile."alizidi kuongea huku akilia kwa kufina fina,aliniacha na lundo la maswali ambayo nikimshushia ni zaidi ya police.

"Ally ndio nani na amefanya nini,?"

"Gao sikuwahi kukwambia, kabla kuwa nina mpenzi anaeitwa ally."

"ndio hujanambia sasa ally ni nani na unalia nini.?"niliendelea na upolice wangu, ambao haukuwa rasmi.

"Gao naomba  tukakae, nikuambie ila inaniuma sana," Alisema, na kukaa sehemu kisha akaanza kunielezea, japo siku hiyo ilikuwa ya kuanza mitihani ya mwezi wa sita, hiyo haikuwa sababu ya kutoacha kuniambia , tukaa pembeni huku nikijaribu kuubana mkojo uliokuwa umenibana, ndio Grace akaanza kunielezea.

"Gao mimi siamini nilikuwa na mpenzi wangu ambaye tulijuana kabla sijahamia shule hii, mana nilikuwa nasoma shule jirani ila mpenzi wangu anasoma shule hii tena kidato cha nne, mwanzoni alinipenda na kunisikiliza kwa kila nitakacho mwambia tulipendana sana ila wiki mbili za nyuma hapo mwenzangu kaanza kubadilika kiasi kwamba hata simu hanipigii wala hanitumii jumbe, hali ile ilikuwa kila siku nikimwambia anachonijibu ni kuwa busy, iliniuma sana nikikumbuka upendo wake wa mwanzo na sasa  haupo tena ule upendo.."akanyamaza kidogo na kuanza kulia hapo mimi nikiyafuta machozi yake kwa reso yangu nyekundu yenye picha ya nembo ya club ya manchester united, nilimbembeleza asilie mana alilia kwa uchungu sana, hali iliyonitia simanzi na mimi nikimuonea huruma.

"Gao, najuta kuwa nae pengine nisingekuwa naye leo hii nisingelia hivyi, Ally ni mwanaume wangu wa kwanza kuwa nae naweza dirikibkuswma yeye ndio alinitoa usichana wangu, kitendo alichonifanyia ally kimeniumiza sana sikuwahi kumsariti tokea niwe nae ila yeye amenisariti na kunifokea kisha kunitamkia matusi ya nguoni."alizidi kuongea huku bado akilia na kunipa kazi ya kumfuta machozi ila kabla hajaendelea tukiwa tumekaa ndipo tukasikia sauti.

"'form three wote mnaitwa mtuhani unaanza'iliita sauti ya mdada ambae ni kiongozi (kilanja) anasoma kidato cha tatu mkondo A huku mimi na Grace tukisoma mkondo B nilimwambia GRACE atangulie kisha mimi nikaelekea msalani kukinusuru kibofu changu kilichoanza kuchoma kutokana na kuubana mkojo,grace alikuwa mmyonge hata tembea yake.
Nilimsindikiza na macho kidogo kisha nikaelekea chooni kukinusuru kibofu changu  kilichokuwa kikichoma kwa kukaa na mkojo muda mrefu, hivyo ilinibidi tu nikajisaidie hapo niliingia chooni na kumaliza haja yangu bila kujali siku hiyo tuna mtihani niliondoka nikitembea mwendo wa kawaida kama sio wa mtu anayewahi kwenda sehemu nilipofika kwenye korido ya madarasa  ya kidato cha nne nilikuta pametulia hakuna kelele wala mwanafunzi anaezunguka pale, hali hiyo iliyofanya nitembe upesi upesi niwahi darasani  mana niligundua mtihani ushaanza kama mwalimu alivyotuamhia.
Nilifika mlango wa chumba changu cha mtihani hapo moja kwa moja nilikutana na msimamizi wa kike mwalimu wa kidato cha kwanza.
Nikaomba kuingia nae bila hiyana akaniruhusu huku akiwa busy na simu yake ya kufuta, wala hakunijali ila aliniambia tu nichukue karatasi ya kufanyia mtihani zilizokuwa mbele pale na mimi nikachukua la maswali na la kujibia kisha nikaanza kukifata kiti changu na meza nikijua vipo kumbe laahasha, nilitizamana na Grace aliekuwa anasimanzi machoni,
Nilimtizama na kumpotezea kisha safari ikaendelea, nilishangazwa nilipofika eneo langu ninalo kaa akiwa amekaa mtu mwengine na meza pamoja na kiti changu havipo ambavyo niliviandika jina vyote jina la GAO DE SWAGGERBOY.
Sikuviona na eneo langu, akiwa amekaa mtu mwengine nilishindwa hata kumsumbua nikabaki nimesimama huku nimeduwaa.
"Wewe mbona umesimama hapo hukai, hujui kama muda haukusubiri nusu saa ishakatika sasa,"alisema msimamizi yule.

"Madam kiti changu na meza sivioni,"nilimjibu.

"Sasa si ukatafute  unachopoteza muda ni nini."alisema madam hapo sikuwa na sababu ya kuendelea kukaa, nilitoka nje kimya kimya kwenda kutafuta kiti na meza, nilizunguka maeneo kadhaa nikitafuta meza kwanza nilikosa, ila nikatazama juu kule ofisini kwa walimu nikafanikiwa kukiona kiti nikiamua nikifate ila kabla sijakibeba alitokea sir lusinde huku kashika lim.

"Gao, mtihani ukiisha nitafute usingoje nikakutafuta hutafanya mtihani wa pili."alinitisha na kuondoka hapo akilibl yangu ilicheza nikajua ni kitendo cha kumtoroka siku ya ijumaa,niliacha kumuwaza kisha nikajibebea kiti nikawa nakishusha kuelekea darasani, kimya kimya nikatafuta eneo nikakaa nikiwa na karatasi zangu.
Kusema ukweli sikuwa nikijua ni mtihani gani tunafanya hata kusoma sijasoma kabisa, yote ni kuondoka bila lidhaa ya muda maalum wa kutoka shule, ndio mana sijapata hata kujua mtihani wa kwanza.
Wakati huo msimamizi alishatangaza imebaki nusu saa hapo sasa ndio nikauangalia mtihani ambao nilikuja ujua ni wa hisabati, hapo kichwa kilipata moto nikiangalia maswali hakuna ninalo kumbuka,nilichofanya nikayacopy maswali yote na kundika jina langu, sikujibu swali hata moja.
Mpaka muda unaisha tukakusanya kisha wote tukatoka tukiwa nje, wanafunzi wenzangu walianza kujidai kila mmoja, wakisema maswali waliyoyajibu hapo mimi nikiwa sina lolote hadi kukaa mbali nao nikimtafuta Grace, hata aniendelezee sikumuona.
Nilipokuwa nimekaa juu ya jiwe ndio nikakumbuka sir lusinde aliniita, Sikujali nilikaa tu pale nikikumbuka kisanga cha yule mkulya nikiogopa sana, ila sidhani kama ninachakupinga juu ya hisia zangu, nilikaa dakika kadhaa kisha ndio nikauliza mtihani unaofatia, nilimuuliza mwanafunzi mwenzangu aliekuwa akipita eneo lile, nae akanijibu ni kiswahili.
nilitumia muda huo kupitia tulivyosoma hasa mambo ya ngeli za maneno,vishazi, aina za maneno, historia ya kiswahili na topic ndogo nyingine, nilikuwa nikisoma ila sijaona kama naelewa, kichwa kilikataa mawazo mengi nilichoamua nibkuelekea vibanda vya chai angalau akili itakaa sawa, nilifika kweli na kunywa chai kisha kurudi juu ile kufika kikagongwa kipindi kumaanisha mtihani umeanza.
Kabla sijakifikia chumba cha mtihani lusinde alikuwa makini nilimuona akishuka haraka haraka kuja darasani kwangu na kwapani kahifadhi fimbo..............
ITAENDELEAAAAAAAA.

INAPATIKANA YOTE FULL LEO LEO WASILIANA NAMI HAPA 0654387935

1 comment:

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();