kotii

kotii

Nuh Mziwanda alipiwa kodi ya nyumba na Shilole

BURUDANI KIGANJANI MWAKO. TANGAZA NASI SASA......


June 22, 2017 kupitia XXL ya Clouds FM mtangazaji Soudy Brown ametusogezea U HEARD ambayo inamuhusu mwimbaji wa Bongofleva Nuh Mziwanda ambaye inadaiwa kodi ya nyumba anayoishi na familia yake amelipiwa na aliyekuwa mpenzi wake Shilole.

Kufuatia kusambaa kwa taarifa hizo Soudy Brown alipiga story na Nawal ambaye ni mke wa Nuh Mziwanda na kusema haimuhusu akidai kitendo hiko ni vizuri kwa kuwa kinampunguzia mumewe majukumu na haimuumizi bali anaangalia maisha yake.

Kwangu mimi naona vizuri inampungumzia mume wangu majukumu kwa sababu ana majukumu mengi; amuangalie mtoto wake, mkewe, familia, bado yeye mwenyewe. Kwa hiyo hata kama yeye akilipa kodi hainiumi hata kidogo. Mimi naangalia maisha yangu.” – Nawal.

No comments

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();